Shirika hilo la Southwest lilisema kuwa
Khairuldeen Makhzoomi aliondolewa tarehe 9 mwezi Aprili baada ya ndege hiyo
kupaa.
Bwana Makhzoomi anasema alikuwa
akizungumza na mjomba wake kwa njia ya simu kuhusu hotuba ya katibu mkuu wa
umoja wa mataifa Ban Ki-moon.
Bwana Nmakhzoomi anasema kuwa mwanamke
mmoja kwenye ndege hiyo alimkodolea macho wakati alitumia jina
"inshallah" akimaanisha Mungu akipenda.
Baada ya kutumia jina hili mfanyikaziawa
shirika la Southwest alimsindikiza nje ya ndege.
Bwana Makhzoomi ambaye aliingia nchini
Marekani kama mkimbizi kutoka Iraq na sasa ni mwanafunzi wa chuo cha Carlifonia
cha Berkeley , aliambiwa kuwa hawezi kuingia kwenye ndege hiyo.
Kutoka BBC Swahili.
0 maoni:
Post a Comment