MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UTENDAJI WA SEKRETARIETI YA AJIRA

Kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa imeipongeza Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa kujitahidi kutekeleza vyema majukumu yake licha ya kukabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ya ufinyu wa bajeti.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mhe. Venance Mwamoto wakati akichangia majadiliano baina ya kamati na Menejimenti ya taasisi hiyo.

Aidha, aliongeza kuwa kamati yake imeweza kuona hali halisi ya kiutendaji, hivyo atamfikishia mwenyekiti wake ili waweze kuona namna kamati hiyo itakavyoweza kutatua changamoto hizo kwa pamoja kwa lengo la kuiwezesha Sekretarieti ya Ajira kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi zaidi.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Wajumbe wa Sekretarieti ya Ajira Bw. Bakari Mahiza wakati akiikaribisha kamati hiyo,  mbali na kuwashukuru na kuwapongeza kwa kuchaguliwa kusimamia sekta hii nyeti inayosimamia rasimaliwatu ambayo ni muhimu katika taifa lolote.

''Kwa uzoefu wangu, natambua kuwa nchi nyingi zilizoendelea ni zile zilizowekeza katika watumishi wenye sifa, ujuzi, ubunifu na maadili mema ambao wanauwezo wa kukabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo za kisiasa, kijamii na kiuchumi'' Alisema Mahiza.

 Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mhe. Jason Rweikiza wakati akifungua kikao cha kamati yake na Menejimenti hiyo amesema wameamua kutembelea Taaisis hiyo ili kujua namna inavyotekeleza majukumu yake na kuona wanavyoweza kushirikiana kwa pamoja ili kuongeza ufanisi wa chombo hicho.

Nae Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angellah Kairuki ameishukuru kamati hiyo kwa kutembelea Taasisi mbalimbali zilizo chini yake na kuahidi kufanyia kazi ushauri walioutoa ikiwa ni pamoja na kuendelea kutumia fursa mbalimbali ikiwemo makongamano ya taasisi nyingine katika kutoa elimu zaidi kwa umma, kuhakikisha inaendelea kupunguza siku za uendeshaji wa mchakato wa ajira pamoja na kufanya marekebisho ya Sheria mbalimbali zinazohusu masuala ya kiutumishi ili kuweza kuboresha utendaji kazi na kupunguza malalamiko yasiyo na ulazima.


Wakati huohuo, Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma Bw. Xavier Daudi pamoja na kueleza jinsi Mchakato wa Ajira unavyoendeshwa, mafanikio, changamoto na matarajio ya chombo hicho, Pia ameahidi kamati hiyo kufanyia kazi ushauri na maelekezo mbalimbali yaliyotolewa na wajumbe wa kamati hiyo ili kuhakikisha Serikali inapata watumishi wenye sifa, weledi kwa kuzingatia Sera, Sheria, Kanuni na Taratibu.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment