MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

KIPINDUPINDU CHAUA WATU 45 ZANZIBAR



 Zanzibar
Watu zaidi ya 45 wamefariki kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu visiwani Zanzibar katika kipindi cha miezi miwili, shirika la habari la AP limeripoti.

Shirika hilo la habari limemnukuu afisa wa afya visiwani humo anayesema vifo hivyo vimetokea mwezi Machin a Aprili.

Muhammed Dahoma, ambaye ni mkurugenzi wa anayeangazia kuzuia maradhi katika wizara ya afya, anasema watu karibu 3,000 wamelazwa hospitalini baada ya kuugua.

Ameongeza kuwa serikali ya Zanzibar imechukua hatua kukabiliana na mlipuko huo.

Miongoni mwa hatua zilizochukuliwa ni kupiga marufuku uuzaji wa chakula na juisi maeneo ya wazi.

Taarifa kutoka visiwani humo zinasema serikali pia imeamuru kufungwa kwa shule zote kwa muda usiojulikana.

Waziri wa elimu Riziki Pembe Juma, amenukuliwa na shirika la habari la Uchina la Xinhua, akisema uamuzi huo umetolewa baada ya kubainika kwamba wanafunzi ni miongoni mwa watu walioathiriwa zaidi na ugonjwa huo.

BBC Swahili

 
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment