Nchini
Rwanda abiria wanaotumia usafiri wa mabasi mjini Kigali wameanza kusafiri kwa
kutumia mfumo mpya wa kadi za elektroniki kwa kulipia nauli.
Mfumo
huu umewakosesha kazi makondakta huku ukikaribishwa na wamiliki wa kampuni za
mabasi ya abiria kwa kuwasaidia kudhibiti wizi wa pesa uliokuwepo.
Mwandishi
wa BBC aliyeko Kigali Yves Bucyana anasema kila abiria aliye na kadi anauingia
ndani ya basi na kubonyeza kadi yake kwenye mashine maalum iliyobandikwa karibu
na mlango wa basi.
Huo ni
mfumo mpya,unaotumiwa na makampuni mawili tu miongoni mwa makampuni kadhaa ya
mabasi ya abiria mjini Kigali.
chanzo BBC Swahili.
0 maoni:
Post a Comment