Rais Barack Obama
amesema anaunga mkono Uingereza kubaki katika jumuiya ya Umoja wa Ulaya ili
kuweza kuchangia katika vita dhidi ya ugaidi na masuala wahamiaji na utatuzi wa
migogoro ya kiuchumi.
Rais Obama ameyasema
hayo anapoanza ziara yake nchini Uingereza.
Rais Obama amenukuliwa
na gazeti la Uingereza Telegraph, akisema kwamba uanachama wa Uingereza katika
umoja wa Ulaya una umuhimu mkubwa na endapo nchi hiyo itajiondoa katika umoja
huo itapunguza nguvu katika vita dhidi ya ugaidi duniani, suala la wahamiaji na
utatuzi wa matatizo ya kiuchumi.
Uingereza kuamua kuhusu EU
Hata hivyo Obama
amesema anatete hoja ya umoja wa Ulaya kuendelea kama ulivyo badala ya
Uingereza kujitioa,japo kuwa anakabiliwa na upinzani kutoka kwa viongozi wa juu
wa Uingereza wanapiga kampeni kujitoa katika umoja huo.
Naye meya wa mji wa
London Boris Johnson amesema Marekani isingeweza kuuza sehemu ya demokrasia
yake kama ambavyo Uingereza imefanya kwa umoja wa Ulaya.
Hii leo Rais Obama
anatarajiwa kukutana na waziri mkuu wa Uingereza David Cameroon kwa mazungumzo
na baadaye chakula cha mchana na malkia Elizabeth wa Uingereza hii ikiwa ni
siku moja baada ya maadhimisho ya miaka 90 ya kuzaliwa kwake.
Kutoka BBC Swahili
0 maoni:
Post a Comment