MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

UCHAGUZI MKUU KUFANYIKA LEO DJIBOUTI

Raia wa Djibouti leo wanapiga kura kumchagua rais mpya.
Lakini tayari kuna utata kwani baadhi ya vyama vya upinzani vinasusia uchaguzi huo, ishara ya jinsi upinzani umegawanyika hivyo kujipata katika hali hiyo hafifu mbele ya chama tawala cha rais aliyeko madarakani, Ismael Omar Guelleh.
Upinzani umekuwa ukilalamika kwamba serikali, haijaweka mazingira sawa ya ushindani.
Wagombea vinara wa upinzani ni Omar Elmi Kaireh na Mohamed Daoud Chehem, lakini kwa sababu ya kutokuwa na umoja miongoni mwao, watakuwa na kibarua kigumu na wachambuzi wa kisiasa wanasema hawatarajiwi kuung'oa utawala wa rais Ismael Omar Guelleh ambaye amekuwa madarakani tangu 1999.
Rais Guelleh ni rais wa pili tu tangu nchi hiyo ijikomboe kutoka kwa utawala wa kikoloni wa Ufaransa mwaka wa 1977.

Djibouti ni nchi iliyozungukwa na mataifa majirani ya Somalia, Yemen na Eritrea ambayo yamekumbwa na mizozo ya kisiasa.
Kutoka BBC Swahili.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment