Mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani Donald Trump, amekubali mwaliko wa kumtembelea rais wa Mexico Enrique Pena Nieto, Jumatano.
Afisi ya rais huyo imesema mipango ya kufanyika kwa mazungumzo ya faraghani baina ya wawili hao inakaribia kukamilishwa.
Mkutano huo utafanyika muda mfupi kabla ya Bw Trump kutoa hotuba kuhusu uhamiaji nchini Marekani.
kutoka BBC Swahili
0 maoni:
Post a Comment