MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

Yahoo yadukuliwa taarifa za watumiaji wake

 Makao Makuu ya Mtandao wa Yahoo
Mtandao wa Yahoo umethibitisha kuwa wadukuzi wamedukua taarifa za zaidi ya watumiaji milioni mia tano katika akaunti zake za watumiaji.

Hata hivyo Yahoo imesema inaamini kuwa shambulio la kimtandao la mwaka 2014 lilikuwa limefadhiliwa na serikali.

Data zilizoibwa ni pamoja na majina, anuani za barua pepe, namba za simu, tarehe za kuzaliwa na nywila za watumiaji ama (Password). Lakini wadukuzi hao hawakugusa kadi za malipo na taarifa za akaunti za kibenki.
Watumiaji wa mtandao huo wameshauriwa kubadilisha nywila zao (password) zao ili kuepuka udukuzi wa kimtandao.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment