MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

Marekani: Idara ya haki yatetea marufuku ya Trump

Raia wa Yemen waliozuiwa kuingia Marekani na agizo hili wameanza kurudi nchini humo
Haki miliki ya pichaEUROPEAN PHOTOPRESS AGENCY
Image captionRaia wa Yemen waliozuiwa kuingia Marekani na agizo hili wameanza kurudi nchini humo
Idara ya haki nchini Marekani imeitetea marufuku ya usafiri ya rais Donald Trump na kuitaka mahakama ya rufaa kuiruhus kwa usalama wa taifa.
Taarifa ya kurasa 15 ilidai kwamba ilikuwa ni hatua ya halali kwa rais Trump na sio kuwapiga marufuku Waislamu.
Agizo hilo la rais liliwazuia kwa muda wakimbizi wote na wageni kutoka mataifa saba ya Waislamu.

    Kesi ya kuikubali ama kuikataa marufuku hiyo imepangwa kusikizwa siku ya Jumanne.
    Ombi hilo liliwasilishwa katika mahakama ya rufaa ya San Francisco baada ya agizo hilo la Trump kusitishwa na jaji wa mahakama ya kijimbo mjini Washington.
    Jaji huyo alisema kuwa marufuku hiyo ni kinyume na katiba na inadhuru maslahi ya taifa hilo.
    Kufuatia uamuzi huo raia kutoka mataifa saba ya Waislamu ikiwemo Iran, Iraq, Libya, Somalia, Sudan, Syria na Yemen walio na Visa halali waliweza kusafiri kuelekea Marekani.

    Share on Google Plus

    About MWERA AMAZING

    This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
      Blogger Comment

    0 maoni:

    Post a Comment