Mahasimu wa jiji la London Chelsea na Tottenham wamepangwa kukutana katika nusufainali Kombe la FA nchini Uingereza, Arsenal nao wakapangwa kukutana na Manchester City.
Arsenal watakuwa wanacheza nusu fainali Kombe la FA kwa mara ya 29
Nusu fainali zote mbili zitachezewa Wembley wikendi ya 22 na 23.
Chelsea walifuzu kwa kuwafunga Manchester United 1-0 Jumatatu.
Spurs walifika nusu fainali kwa kulaza Millwall 6-0 Jumapili.
Arsenal, ambao walishinda kombe hilo 2014 na 2015 waliwalemea Lincoln City 5-0 Jumamosi.
Manchester City ambao wanacheza nusu fainali kwa mara ya kwanza katika misimu minne, walifuzu kwa kulaza Middlesbrough 2-0 ugenini.
Kutoka BBC Swahili
0 maoni:
Post a Comment