Kiongozi wa chama cha Alliance for Change & Transparency Wazalendo nchini Tanzania Zitto Kabwe amesema waziri wa habari aliyefutwa kazi Bw Nape Nnauye "ni shujaa".
Kwenye Twitter, Bw Kabwe, ambaye ni mbunge wa Kigoma-Ujiji Municipality amesema amewasiliana na Bw Nnauye ambaye amemthibitishia kwamba ni kweli ameondolewa kwenye wadhifa wake wa uwaziri.
Taarifa kutoka ikulu mapema leo ilitangaza waziri mpya wa habari, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuwa Dkt. Harrison George Mwakyembe.
Taarifa hiyo haikusema chochote kuhusu hatima ya Bw Nnauye.
Dkt Mwakyembe amekuwa akihudumu kama Waziri wa Katiba na Sheria.
Bw Nnauye kwenye Twitter amewaomba watu kuwa na subira na kuahidi kwamba atazungumza na wanahabari baadaye leo.
"Ndugu zangu naomba TUTULIE! LEO mchana nitakutana na Wanahabari na tutalizungumza hili. Nitawaambia saa na mahali, kwasasa naomba TUTULIE!" ameandika.
Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) limempongeza Dkt Mwakwembe kufuatia uteuzi wake.
0 maoni:
Post a Comment