MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

Viongozi wa G7 waangazia bara la Afrika

 Viongozi wa G7 wanaliangazia bara la Afrika hususan swala la wahamiaji wanaoingia Afrika
Viongozi kadha wa nchi za Afrika wanahudhuria siku ya pili ya mazungumzo katika mkutano huo wa G7, ili kujadili tatizo la wahamiaji.

Itali iliamua kuandaa mkutano huo huko Sicily, ili kuvutia macho ya ulimwengu juu ya shida za Waafrika wanaohatarisha maisha yao, kuvuka Mediterranean ili kuingia Ulaya.

Tayari mwaka huu, wahamiaji elfu hamsini wameingia Italia, huku 1500 wamezama safarini.

Kwa hivyo viongozi wa G7 wamezungumza na wenzao kutoka Tunisia, Kenya, Ethiopia, Niger na Nigeria, kutafuta njia za kuhimiza maendeleo Afrika, ikitarajiwa kuwa itawafanya wahamiaji wabaki makwao.

Lakini juhudi za Itali, za kutaka G7 kukubali kupokea wahamiaji zaidi, inaelekea zitapingwa na hasa Marekani.

kutoka BBC Swahili
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment