K.NYAMWASA AAKIWA KUVULIWA UKIMBIZI
Mashirika mawili ya kutetea haki za binadamu yameiomba mahakama moja ya Afrika Kusini kutoa amri ya kumvua hadhi ya ukimbizi aliyekuwa mkuu wa majeshi ya Rwanda Faustin Nyamwasa.
Mashirika hayo yanadai kuwa Uhispania na Ufaransa zina vibali vya kumchukua Generali Faustin Nyamwasa, na kumsafirisha katika nchi hizo kukabiliwa na sheria.
Aidha mashirika hayo yanasema kuwa Generali Nyamwasa anakabiliwa na tuhuma za kuhusika katika mauaji ya raia nchini Rwanda na Congo na kwa hivyo hafai kulindwa na sheria ya wakimbizi nchini Afrika Kusini.

0 maoni:
Post a Comment