MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

Baada ya titi tutaoneshwa nini?


           KWA tamaduni za makabila mengi Tanzania titi la mwanamke limepewa thamani na kuchukuliwa kama kiungo cha faragha. Halipaswi kuonyeshwa hadharani.
 Titi si kiungo kinachopaswa kuachwa wazi ili kila mwenye jicho aone. Titi lina mahala pake pa kulionyesha. Na zaidi lina mtu wake anayepaswa kuliona na kuligusa. Tena kwa wakati maalum.

Titi lina sifa kubwa kuu mbili; kwanza kushibisha watoto na pili, kwa watu wengi titi ni kiungo muhimu katika kunogesha mapenzi. Wengine titi wanaliita “chumvi” ya mapenzi – chakula bila chumvi hakinogi. Titi hilo.

Ukimshika mwanamke mkono, mguu, kichwa na hata jicho bila ridhaa yake hawezi kukushitaki. Lakini mguse titi; akikushitaki umefungwa! Ujue titi si kiungo cha kawaida katika mwili wa mwanake.

Lakini siku hizi dada zetu wameacha utamaduni wa kulithamini titi. Imekuwa fasheni kwao kuacha matiti wazi. Kwa mwanamke mwenye kujiheshimu hii ni kashfa kwake. Sijui baada ya titi sehemu gani nyingine nyeti itafuata kuachwa wazi.

Titi linalochukuliwa kama chumvi ya mapenzi halithaminiwi, kutakuwa na ajabu gani tukiona chakula kinachonogeshwa na chumvi nacho kikiachwa wazi?

Wapo dada zetu wanaochora matiti yao na kuyaanika hadharani. Bahati mbaya, wengi wao wanafanya haya kwa kuiga na wala hawajui maana yake.

Titi linachorwa na kuachwa wazi makusudi ili kila mwenye jicho aone. Aliyefikia hatua ya kuonyesha titi wazi usimwamini, siku yoyote ataonyesha sehemu nyingine nyeti.  

Siku hizi kuna sidiria zinazo nyanyua matiti na kuonekana kama jipu linalosubiri kutumbuliwa. Wanaoacha wazi matiti wanafikiri wanaume wanaona wanawafagilia, kumbe wengi wao wanawalaani na kuwadharau.

Wakati wa utoto wangu ilikuwa vigumu kuona titi la msichana likiwa limeachwa wazi. Lakini siku hizi haipiti siku bila kuona matiti ya wasichana yakiwa wazi.
 Utapita wapi usione msichana aliyepiga ‘jeki’ titi na kuliacha wazi? Ukiingia kwenye ofisi nyingi utakutana na  wasichana waliopiga jeki matiti yao. Ukipanda daladala utawakuta wamesimamisha vifua na ukiwa sehemu ya kupata kinywaji huko ndio kabisaa! 

Kuna baadhi ya wanaume wakiona tu titi wanasisimka hata kabla hawajaligusa na wanawake wanalijua hilo. Shaka yangu ni kwamba, wanaume wakizoea kuona matiti na wakaanza kupuuza dada zetu wataamua kutuonyesha sehemu gani nyingine nyeti?

Titi ni miongoni mwa viungo adhimu kwenye mapenzi. Baadhi ya wanaume wanapata msisimko mkubwa wanapogusa titi la mwanamke, na hata baadhi ya wanawake wanapata msisimko wa ajabu wanapoguswa matiti na mwanaume.

Titi lina mvuto wake bwana; kuna titi la dodo, bolibo na hata papai. Lipo pia titi la boga. Kwa baadhi wa wanawake na wanaume wanatumia titi kufikishana kileleni. Titi hilo.

Hata wale wanawake wenye kunyonyesha hadharani hawatakiwi kuliacha wazi titi. Unaweza kumwona mwanamke ananyonyesha mtoto ndani ya daladala na kuliachia titi kila aliyomo ndani ya daladala alione.

Sisemi watoto wakitaka kunyonya kwenye daladala wasinyonyeshwe, la hasha. Ninachosema kuwepo na ustaarabu wa kulificha titi hata wakati wa kunyonyesha. Mbona wanawake wengine wanaweza kunyonyesha mbele za watu na titi lake lisionekane?

Kuna sehemu zake za kuacha titi wazi na kuna watu wake wanaopaswa kuonyeshwa, kuligusa na hata kulichezea. Titi lipewe thamani yake. Sijui baada ya titi tunaonyeshwa nini. Tusubiri.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment