FILAM INAYOMKOSOA RAIS WA UGANDA YAFUNGIWA
Maafisa wa serikali nchini Uganda wamepiga marufuku mchezo wa kuigiza unaokosoa serikali ya Rais wa nchi hiyo Yoweri Museveni.
Mwandishi wa mchezo huo John Ssegawa alisema kuwa baraza la vyombo vya habari liliamuru kusitishwa kwa mchezo huo hadi utakapodurusiwa.
Mchezo huo unaangazia maswala ya ufisadi na uongozi duni nchini Uganda chini ya utawala wa Museveni tangu mwaka 1986.
Mwezi jana, mtengezaji vipindi mmoja alikamatwa nchini humo kwa kuonyesha mchezo wenye mada ya mapenzi ya jinsia moja bila ya idhini na maafisa wakuu.

0 maoni:
Post a Comment