WATOTO WALIPUKIWA NA BOMU TANZANIA
Watoto watano ,watatu wakiwa wa familia moja wamekufa Wilayani Karagwe mkoani Kagera Magharibi mwa Tanzania.
Ni baada ya kulipukiwa na bomu la kutupwa kwa mkono wakati walipokuwa wakichezea Bomu hilo lililookotwa kwenye vyuma chakavu na kudhani kuwa ni mpira.
Tukio hilo lilitokea Jumatano majira ya asubuhi huko Wilayani Karagwe mkoani Kagera Magharibi mwa Tanzania wakati watoto walipokuwa wakichezea kitu mfano wa mpira mdogo ,ambacho baadaye kilikuja kutambulika kuwa lilikuwa Bomu la kurushwa kwa mkono.

0 maoni:
Post a Comment