MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

ABU QATADA
KUBAKI UINGEREZA
 Serikali ya Uingereza hatimaye imeshindwa katika dakika za mwisho kwenye kesi ya kumuondosha nchini hapa mhubiri wa dini ya kiislamu mwenye itikadi kali Abu Qatada kwenda nchini Jordan.
Abu Qatada amekuwa akitakiwa na serikali ya Jordan baada ya kupatikana na hatia ya makosa ya ugaidi mwaka 1999.
Serikali ya Uingereza,imekuwa ikijaribu kumuondoa nchini Uingereza,kiongozi huyo ambaye ni mhubiri wa dini ya kiislamu kwa zaidi ya miaka kumi iliyopita bila mafanikio,baada ya mabishano makubwa ya kisheria.
Hili limekuwa ni anguko jingine kwa Serikali ya Uingereza hasa wizara ya mambo ya ndani, ambapo Mhubiri huyo wa dini ya Kiislamu anayetambulika kisheria kama Omary Mohammed Othman,maarufu kama Abu Qatada,ameendelea kupata kinga ya mahakama ya kusalia nchini Uingereza.
Mahakama ya rufaa mjini London,kwa pamoja imeyakataa maombi ya Waziri wa mambo ya ndani Theresa May,ambaye alipeleka kesi kwa niaba ya Serikali
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment