MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG


SUDANI KUSINI NA SUDAN ZAFIKIA MWAFAKA

Sudan na Sudan Kusini zimeafikia makubaliano kuhusu mgogoro
wa mpaka na uzalishaji wa mafuta.
Baada ya mazungumzo ya siku ya nne, nchi hizo mbili zimeafikiana
 kuruhusu usafirishaji wa mafuta kutoka kusini kupitia mabomba ya
 Kaskazini na kuondoa wanajeshi mpakani.
Viongozi wa nchi hizo mbili hatimaye walikubaliana baada ya
 mazungumzo ya siku nne mjini Addis Ababa Ethiopia.
Lakin maswala kadhaa muhimu yangali kutatuliwa ikiwemo
kuafikia makubaliano kuhusu mipaka inayozozaniwa ikiwa ni
mojawpao ya kilichosababisha mgogoro ambao nusura utumbukize
nchi hizo kwenye vita mapema mwaka huu.
Baada ya mapigano kuzuka kuhusu mzozo wa mafuta na mipaka,
Umoja wa mataifa ulitishia kuziwekea pande zote mbili vikwazo
ikiwa hazitaafikia makubaliano ya kina.
Wapatanishi wa Muungano wa Afrika wangali kuthibitisha kuwa
makubaliano yameafikiwa lakini rais wa Sudan Omar al-Bashir na
 mwenzake wa Kusini Salva Kiir, wanatarajiwa kutia saini
makubaliano hayo hii leo.
Maelezo yametolewa tu kwa mukhtasari lakini wapatanishi
wa pande zote mbili, walisema kuwa wamekubaliana kuhusu eneo la
 nchi hizo mbili ambalo halina ulinzi wa kijeshi.
Pia makubaliano ya kiuchumi yaliafikiwa kuruhusu Sudan Kusini
 kuanza tena shughuli zake za kuzalisha mafuta.
Lakini mwafaka haukupatikana kuhusu eneo linalozozaniwa la Abyei
wala mipaka mingine mingi ambayo nchi hizo zinazozania.
Kwa hivyo makubalino hayo hayajaweza kutimiza masharti ya
Umoja wa Mataifa kwa nchi hizo kuafikia mkataba unaotatua mzozo huo kwa kina
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment