MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

WANAFUNZI 20 WAUAWA NA BOKO HARAM
Takriban wanafunzi 20 wameuawa kwa kupigwa risasi katika eneo
 la Mubi, Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.

Polisi wamefahamisha BBC kuwa shambulizi hilo limetokea katika
 dahalia ya wanafunzo(Hostel) mbali kidogo na chuo cha ufundi anuwai
cha Mubi.
Mhadhiri mmoja amefahamisha BBC kuwa wanafunzi 40 wameuawa
lakini bado taarifa hizo hazijathibitishwa.
Mauaji haya yanakuja siku chache baada ya operesheni kali kufanywa
dhidi ya kundi la wapiganaji wa kiisilamu la Boko Haram mjini humo.
Aidha mhadhiri ambaye hakutaka kutajwa, aliambia BBC kwamba
wanafunzi waliamrishwa kupanga foleni na kusema majina yao mmoja
 baada ya mwingine kabla ya kuuawa.
Haijulikani kwa nini baadhi waliuawa na wengine kuachwa, baadhi
ya wale waliouawa ni waisilamu.
"kila mtu anaogopa na wamejifungia vyumbani," alisema mhadhiri huyo.
Aliongeza kuwa wanafunzi sasa wameanza kuuhama mji huo.
 Inasemekana wameweka majani ya rangi ya kijani kibichi kwenye
magari yao kama ishara kuwa hawaungi mkono upande wowote.
Wapiganaji wa Boko Haram wanaopigana wakitaka sheria za kiisilamu
kutumika, wamewaua zaidi ya watu 1,000 Kaskazini mwa Nigeria.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment