Mamlaka nchini Ethiopia wanadaiwa kuwatesa na kuwatendea vibaya mahabusu
wa kisiasa kwa lengo la kuwalazimisha kukiri makosa Shirika la Kimataifa la
Haki za Binadamu la Human Right Watch limesema.
Shirika hilo lenye makao yake nchini Marekani limesema wafungwa
walishikiliwa katika mahabusu kuu katikati ya mji mkuu wa Adis Ababa wamesema
wamekuwa wakichapwa na kupigwa mateke wakati wa mahojiano.
Shirika hilo linaishutumu Ethiopia kwa kutumia sheria ya kupinga
Ugaidi kuwakandamiza wapinzani.
Hata hivyo serikali ya Ethiopia imetupilia mbali madai ya ripoti
hiyo na kusema kuwa imeegemea upande mmoja na kukosa ushahidi wa kutosha,
Shirika la Habari la AP limesema.
Ripoti ya Shirika hilo la Haki za binadamu limesema polisi
wanaofanya upepelezi katika gereza la Maekelawi wamekuwa wakitumia njia haramu
za kuwahoji watuhumiwa, kuwaweka wafungwa walioshikiliwa katika mazingira
mabaya na kuwazua kuwasiliana na wanasheria.
Mmoja kati ya mahabusu amenukuliwa akisema " amekuwa
akishikiliwa katika eneo la mateso kwa masaa kadhaa, kuning'inizwa kwenye ukuta
wakati akipigwa bakora", taarifa hiyo imesema.
Kutoka BBC
0 maoni:
Post a Comment