Shughuli ya kutafuta ndege ya abiria ya Malaysia
imeendelea kushika kasi baada ya kuwepo kwa hali ya suitofahamu na wasiwasi
mwingi kutoka kwa ndugu za watu waliopotea wakiwa katika ndege hiyo................
Mamlaka nchini Malaysia zinasema wameongeza mipaka ya
eneo la utafutaji, mara mbili Zaidi, huku China ikiwa imepeleka mitambo 10 ya
satelaiti kwa ajili ya kusaidia kutafuta ndege hiyo.
Mkuu wa Idara ya anga Azharuddin AbdulRahman
amewaambia waandishi wa habari kuwa eneo la kusaka ndege hiyo limeongezeka mara
mbili kutoka maili 50 za baharini kunakosemekana ndege ilipotelea mpaka maili
100.
Ndege iliyokua imebeba watu 239 ilipotea bila kutoa
taarifa yeyote na hakuna dalili yeyote mpaka sasa ya kupatikana kwa mabaki ya
ndege hiyo.
0 maoni:
Post a Comment