MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

MAREKANI YASIKITISHWA NA UMOJA PALESTINA



 Marekani yasikitishwa na umoja Palestina
Marekani inasema imesikitishwa na makubaliano kati ya makundi makuu Palestina ya kuiunda serikali ya Umoja...............

           
Imeoya huenda hatua hiyo ikatatiza zaidi jitihada za amani. Uamuzi huo unalijumuisha kundi lenye msimamo kali za kidini, Hamas, unaliotawala eneo la Gaza na limetajwa na Marekani na Israeli kama kundi la kigaidi.

Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni wa Marekani Jen Psaki amesema wakati wa kutangaza uamuzi hduo ndio unaotia wasiwasi.

Tangazo hilo limefanywa wakati ambapo Marekani ilikuwa ikijitahidi kushawishi Israil na Wapalestina kukubali kuendelea kufanya mashauriano ya amani ambayo hadi kufikia sasa hayajazaa matunda yo yote.
 
Bi Psaki amesema mapatano kati ya Wapalestina yatavuruga vibaya sana juhudi hizo na akatangaza kuwa itakuwa vigumu kwa Israil kufanya mashauriano nakundi ambalo haliamini kuwa Israili ina haki ya kuwepo kama taifa; jinsi wanavyoamini wanachama wa Hamas.

Alisema Serikali ya Marekani itaendelea kuchunguza kwa makili hatua zinazochukuliwa kuhusiana na uamuzi huo na Wapalestina siku na hata masaa yanayokuja.

Wamarekani na mataifa washirika wake wamesisistiza kuwa muda mrefu kuwa taifa lo lote la Wapalastina inapaswa kuwa lile linaloshutumua vita, litambue Israil na kukubalia mapatano yote yanayohusisha taifa hilo la Wayahudi.

Wapalestina wanasisitiza kuwa umoja wao utampa uhalali zaidi Rais Mahmoud Abbas, kufanya mashauriano kwa niaba yao kwa sababu atakuwa akiwakilisha Wapalestina wote na wala sio baadhi yao tu.
kutoka BBC
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment