Serikali
ya Mali na
makundi sita ya wanamgambo wanatarajiwa kutia sahihi makubaliano ya amani yenye
nia ya kuleta utulivu nchini humo..............
Chini
ya makubaliano hayo wanamgambo hao watajumuishwa kwenye jeshi la Mali na
kutumwa eneo la kaskazi mwa nchi .
Vikosi
vya ufaransa na vingine kutoka nchi za Afrika vilingia nchini Mali mwezi
Januari mwaka 2013 kuzuia kuenea kwa wanamgambo walio na uhusiano na mtandao wa
al Qaeda kwenda maeneo ya kusini .
Wanamgambo
hao walitimuliwa kutoka miji iliyo kaskazini mwa nchi lakini hata hivyo wale
walio wafugaji wa Tuareg na makundi mengine ya kiislamu bado yanaendelea na
harakati zao.
Kusainiwa
makubaliano hayo kunafanyika baada ya baraza la usalama la umoja wa mataifa
kutoa vitisho vya vikwazo kwa waasi wa Tuareg na makundi yanayoiunga mkono
serikali.
Kutoka BBC
0 maoni:
Post a Comment