Askari polisi mzungu
aliyemburura mwanafunzi mweusi huko Marekani alipokaidi amri ya mwalimu ya
kumtaka apeane simu yake amefutwa kazi.
Ben Fields, amepigwa
chini na jimbo la South Carolina baada ya video kusambazwa katika mitandao ya
kijamii ikimuonesha akimburura msichana mweusi mwanafunzi wa shule ya Spring
Valley ,Columbia.
Katika video
hiyo,Fields anaonekana akimtosa binti huyo sakafuni kwa nguvu na kisha kumbana
kama vile wanavyobanwa magaidi wanapokamatwa na polisi.
Yamkini Fields aliitwa
na mwalimu ambaye alikuwa akifunza kisha akamfumania mwanafunzi huyo akitumia
simu yake darasani kinyume cha sheria.
Mwanafunzi huyo
alikaidi amri ya kupeana simu hiyo ama kuondoka darasani.
Mwanafunzi mwenzake
ndiye aliyechukua video ya tukio hilo
Kauli hiyo
ilimgadhabisha mno mwalimu huyo na kusababisha atafute msaada kutoka kwa askari
huyo.
Hapo ndipo Fields
alitumia nguvu kupita kiasi dhidi ya mwanafunzi huyo wa kike alipokataa
kuondoka darasani.
Fields alimweleza kuwa
amemkamata.
Alimtosa chini kwa
nguvu.
Mwanafunzi mwenzake
ndiye aliyechukua video ya tukio hilo kwa simu na kusambaza kwenye mitandao ya
kijamii.
Tukio hilo limeibua
hisia kali huku wanaharakati wa kupigania haki za watu weusi nchini Marekani
wakidai kuwa afisa huyo wa polisi alitumia nguvu kupita kiasi kwa sababu
alikuwa ni mwanafunzi mweusi.
Aidha makundi ya wazazi
pia wamelalamikia matumizi ya polisi dhidi ya wanafunzi
KUTOKA BBC
0 maoni:
Post a Comment