Marekani imelaani hatua
ya tume ya uchaguzi ya Zanzibar ZEC ya kufuta matokeo ya uchaguzi wa rais
pamoja na wajumbe wa bunge la wawakilishi visiwani humo.
Katika taarifa
iliyowekwa kwenye mtandao wa ubalozi huo nchini Tanzania, Marekani ilisema
imeshtushwa na hatua hiyo na kutoa wito tume hiyo iondoe tamko hilo.
Zec imeahidi kutangaza
tarehe mpya ya marudio ya uchaguzi huo.
Katika kufutilia mbali
matokeo ya urais wa Zanzibar, tume ya uchaguzi ya Zanzibar-ZEC ilisema shughuli
nzima ya upigaji kura visiwani iligubikwa na kasoro nyingi.
Mwenyekiti wa Tume ya
Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Jecha Salim Jecha amesema baadhi ya makamishna wa tume
hiyo, badala ya kutekeleza majukumu yao inavyotakiwa kikatiba "wamekuwa ni
wawakilishi wa vyama vyao".
"Kumegundulika
kasoro nyingi katika uchaguzi huu miongoni mwa hizo ni kubainika kwa baadhi ya
vituo hasa Pemba vimekuwa na kura nyingi kuliko daftari la wapiga kura wa kituo
husika."
Amesema hilo ni jambo
la kushangaza ikizingatiwa kwamba "baadhi ya wapiga kura hawakwenda
kuchukua vitambulisho vyao vya kupigia kura".
Kadhalika, amesema kura
hazikupata ulinzi mzuri hususan kisiwani Pemba ambako amesema kuwa baadhi ya
mawakala wa baadhi ya vya vyama vya siasa katika kisiwa hicho walifukuzwa.
Hata hivyo, taarifa ya
ubalozi wa Marekani inasema kufutilia mbali matokeo hayo kunasitisha mchakato
wa uchaguzi uliofanyika vizuri na kwa amani.
Aidha Taarifa hiyo
inasema kuwa hatua hiyo ya tume ya uchaguzi ya
Zanzibar inakwenda kinyume
kabisa na tathmini ya waangalizi wa uchaguzi kutoka ubalozi wa Marekani,
jumuiya ya ulaya, jumuiya ya madola na jumui ya ya maendeleo ya nchi za kusini
mwa Afrika, SADC kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa haki
KUTOKA BBC
0 maoni:
Post a Comment