MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

MAGAIDI WALIJIFANYA WAHAMIAJI:UFARANSA

Waziri mkuu wa Ufaransa,Manuel Valls, amesema kwamba watu wanaohusishwa na kundi la Islamic State ambao walitekeleza shambulizi mjini Paris wiki iliyopita,ambalo liligharimu uhai wa watu mia moja na ishirini na tisa,waliingia nchini humo kwa mgongo wa sakata la uhamiaji barani ulaya na kuzamia nchini Ufaransa bila kugundulika.

Ameyasema hayo wakati alipokuwa anazungumza katika runinga ya taifa hilo na kwamba wahusika wengine wa ugaidi walikuwemo katika nchi za Ufaransa na Ubelgiji mapema.


Waziri huyo aliongeza kuwa haikufahamika mara moja kwamba kulikuwa na makundi ya namna hiyo kwa ukubwa wake ,ama mshukiwa Salah Abdeslam, ambaye ndiye hasa kielelezo cha mwanamume anayesakwa zaidi kimataifa na haikujulikana kama alikuwa Ubelgiji ama Ufaransa.

CHANZO BBCSwahili
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment