MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

MAREKANI YATOA TAHADHARI

Serikali ya Marekani imetoa tahadhari ya kusafiri duniani kote kwa raia wake, ikiwaonya kuwepo kwa ongezeko la tishio la kigaidi.

Tahadhari hiyo inasema taarifa zilizopo hivi sasa zinaashiria kwamba makundi kama vile Islamic State, al-Qaeda na Boko Haram wanaendelea 
kupanga mashambulio katika maeneo tofauti.

Inawataka wasafiri kuwa makini hasa wanapokuwa katika mikusanyiko ya watu au pindi wanapotumia usafiri wa umma.

Hata hivyo, afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ameiambia bbc kwamba hakuna sababu ya kuamini kwamba raia wa Marekani ndio walengwa.


Mamilioni ya raia wa marekani watasafiri wiki hii kwa ajili ya sikukuu ya kutoa shukrani siku ya alhamisi.

kutoka BBC Swahili
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment