MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

KOREA KASKAZINI KUFANYIA MAJARIBIO NYUKLIA

Korea Kaskazini
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un ametangaza kwamba taifa hilo litafanyia majaribio silaha za nyuklia na makombora ya masafa marefu karibuni.
Amesema majaribio hayo yataimarisha uwezo wa taifa hilo kutekeleza mashambulio ya nyuklia, vyombo vya habari vya serikali nchini humo vimeripoti.
Kim Jong-un ametoa tangazo lake la karibuni zaidi alipokuwa akiongoza maonesho mwigo ya teknolojia ambayo inahitajika kuwezesha kombora lenye kilipuzi cha nyuklia kuingia tena ardhini baada ya kurushwa anga za juu, shirika la habari la KCNA limeripoti.
Shirika hilo limemnukuu akisema majaribio hayo yatafanyika “karibuni” lakini hakusema ni lini.
Korea Kaskazini imekuwa ikitoa msururu wa vitisho baada ya kuwekewa vikwazo vipya na Umoja wa Mataifa.
Lakini ingawa inajulikana kuwa ina silaha za nyuklia, wengi wanashuku uwezo wake wa kuzitumia.

Wiki iliyopita, Bw Kim alidai wanasayansi wa taifa hilo walikuwa wamefanikiwa kuunda kilipuzi cha nyuklia kidogo sana ambacho kinaweza kuwekwa kwenye makombora ya masafa marefu.
kutoka BBC Swahili
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment