Amesema majaribio hayo yataimarisha
uwezo wa taifa hilo kutekeleza mashambulio ya nyuklia, vyombo vya habari vya
serikali nchini humo vimeripoti.
Kim Jong-un ametoa tangazo lake la
karibuni zaidi alipokuwa akiongoza maonesho mwigo ya teknolojia ambayo
inahitajika kuwezesha kombora lenye kilipuzi cha nyuklia kuingia tena ardhini
baada ya kurushwa anga za juu, shirika la habari la KCNA limeripoti.
Shirika hilo limemnukuu akisema
majaribio hayo yatafanyika “karibuni” lakini hakusema ni lini.
Korea Kaskazini imekuwa ikitoa msururu wa
vitisho baada ya kuwekewa vikwazo vipya na Umoja wa Mataifa.
Lakini ingawa inajulikana kuwa ina
silaha za nyuklia, wengi wanashuku uwezo wake wa kuzitumia.
Wiki iliyopita, Bw Kim alidai
wanasayansi wa taifa hilo walikuwa wamefanikiwa kuunda kilipuzi cha nyuklia
kidogo sana ambacho kinaweza kuwekwa kwenye makombora ya masafa marefu.
kutoka BBC Swahili
0 maoni:
Post a Comment