Umoja wa Milki za
Kirabau umesema ndege yake ya moja ya kivita imetoweka ikitekeleza mashambulio
dhidi ya waasi wa Houthi nchini Yemen.
Shirika la habari la
serikali ya nchi hiyo, WAM, lilitangaza kutoweka kwa ndege hiyo bila kutoa
maelezo zaidi.
UAE imekuwa ikishiriki
katika mashambulio ya muungano wa mataifa yanayoongozwa na Saudi Arabia
kutekeleza mashambulio ya angani
kumuunga mkono Rais Abedrabbo Mansour Hadi
tangu Machi 2015.
Watu 6,000 wameauawa
kwenye mapigano nchini Yemen.
Hicho ndicho kisa cha
kwanza cha kutoweka kwa ndege ya UAE kwenye mapigano hayo.
Maafisa bado
hayajaeleza ndege iliyotoweka ni ya muundo gani na pia iwapo marubani
walidhurika.
Jeshi la wanahewa la
UAE hutumia ndege za kivita aina ya F-16 na Mirage 2000.
Desemba, ndege aina ya
F-16 ya jeshi la Bahrain ilianguka Saudi Arabia kutokana na “hitilafu za
kimitambo”, na mwezi Mei ndege ya kivita ya Morocco ilitunguliwa nchini Yemen.
Ndege hizo mbili
zilikuwa zikishiriki mashambulio dhidi ya waasi wa Houthi.
kutoka BBC Swahili
0 maoni:
Post a Comment