Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe alikutana na Askofu mkuu wa
Canterbury na kuibua maswali kuhusu ndoa za wapenzi wa jinsia moja.
Askofu mkuu Justin Welby amesema alimjibu kiongozi huyo kwamba
kuna mitazamo tofauti kuhusu ndoa hizo miongoni mwa waumini wa kanisa la
Kianglikana kote duniani.
Aliongeza hata hivyo kwamba wengi wa waumini wanaamini ndoa ni
uhusiano wa muda mrefu baina ya mwanamume na mwanamke.
Askofu Welby alisema ni makosa kuwahukumu au kuwaadhibu watu kwa
sababu ya msimamo wao kijinsia na kimapenzi.
Hata hivyo, amesema dalili zilionesha Bw Mugabe hakukubaliana
naye.
“Sidhani itakuwa haki kusema kwamba Bw Mugabe alikubaliana name
kabisa,” alisema Askofu Welby.
kutoka BBC Swahili
0 maoni:
Post a Comment