MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

VIONGOZI KUJADILI UHIFADHI WA NDOVU AFRIKA



Kenya


Viongozi watatu wa nchi za Afrika wanakutana leo nchini Kenya kujadili njia za kuokoa ndovu ambao wanakabiliwa na tishio la kuangamia kutokana na ujangili.

Mkutano huo wa kwanza wa viongozi na watu mashuhuri duniani ambao unajulikana kama mkutano wa Giants Club utaongozwa na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.

Mkutano huo pia utawashirikishia viongozi wa makundi ya uhifadhi wa wanyama, wafanyabiashara na wanasayansi.

Kabla ya kufanyika kwa mkutano huo, Rais Kenyatta amesema ametoa wito kwa hatua madhubuti kuchukuliwa dhidi ya biashara haramu ya pembe.

Rais Kenyatta amesema kuwa ndovu wanakabiliwa na hatari ya kuangamizwa na kizazi kipya cha wawindaji haramu, waliojihami vilivo na walio na uhusiano wa kimataifa, na matokeo yake yamekuwa mabaya sana.

Wataalamu wanasema idadi ya ndovu Afrika ilishuka kwa asilimia 90 karne iliyopita na wanaonya kuwa huenda wanyama hao wakaangamia katika miongo kadha ijayo.

Kutoka BBC swahili


Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment