Rais wa Marekani Donald Trump
alifichua taarifa zinazofaa kuwa siri kuu kuhusu kundi linalojiita
Islamic State (IS) kwa waziri wa mambo ya nje wa urusi, vyombo vya
habari nchini Marekani vinasema.
Bw Trump alikutana na Sergei Lavrov katika afisi yake wiki iliyopita.
Mshauri mkuu wa usalama wa taifa wa Marekani HR McMaster amepuuzilia mbali madai hayo kwenye vyombo vya habari na kusema ni ya "uongo".
Tuhuma kwamba huenda maafisa wa kampeni wa Bw Trump waliwasiliana na maafisa wa Urusi zimegubika utawala wa rais huyo, na kufikia sasa uchunguzi unaendelea.
0 maoni:
Post a Comment