MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

AFRIKA KUSINI YATANGAZA KIKOSI CHAKE


Timu ya taifa ya soka ya Afrika Kusini, imetangaza kikosi chake ambacho kitapambana na Zambia katika mechi ya kirafiki.
Afrika Kusini imeamua kuwaalika wachezaji wake nchini Ubelgiji, Darren Keet na Anele Ngcongca katika mechi hiyo dhidi ya mabingwa wa Afrika, Zambai.

Pambano hilo litachezwa tarehe 14 mwezi Novemba.
Keet ni kati ya walinda lango wawili wa timu hiyo, naye mlinzi wa timu ya Genk, Ngcongca, amechaguliwa kwa mara ya kwanza na kocha wa timu ya taifa, Gordon Igesund.
Kufuatia Steven Pienaar kustaafu kutoka mechi za kimataifa, mlinzi wa zamani wa Tottenham ya Uingereza, Bongani Khumalo, sasa ataiongoza timu hiyo kama nahodha.

Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment