MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

KENYA YAWEKA SHERIA MPYA YA NDOA



Baraza la mawaziri nchini Kenya linapendekeza mabadiliko makubwa kwa sheria za ndoa nchini humo .
Mswaada wawaliowasilisha unapendekeza kuwa wanaume wanweza kuoa zaidi ya mke mmoja na hata kuharamisha mahari ambapo familia ya mwanaume inalipa mahari hiyo.
Pia inataka kuhalalisha watu kuishi pamoja kama mume na mke bila ya ndoa kwa kipindi cha miezi sita kama njia ya kulinda watoto na wanwake wakati uhusiano huo unapovunjika.

Mapendekezo hayo tayari yamezua hisia kali kutoka kwa jamii kwa ujumla. Aidha mswaada huo, lazima uidhinishwe na bunge kabla ya kufanywa sheria.
Wengi wa wanaoishi maisha kama hayo ni wanafunzi wa vyuo vikuu ambapo uhusianao kama huo unajulikana kama "come we stay" au njoo tuishi pamoja kama mke na mume bila ya ndoa.
Wanafunzi hujipata katika uhusiano kama huo kwa hata miaka minne au zaidi wakati wakisoma na punde baada ya kuhitimu , huvunja uhusiano ule.
Mara nyingi watu huishi pamoja bila ya kuoana kwa sababu za manufaa ya ule uhusiano
Wakati mwingine hata hupata watoto wakati wa kipindi kile wanapoishi pamoja , na hapo ndipo mwanamue hutafuta njia za kutoroka ili kukwepa majukumu yake.

Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment