MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

MAGEUZI YAFANYIKA CHINA

Rais wa China Hu Jintao amefungua rasmi kongamano la chama tawala ambalo linaanza mfumo mpya wa utawala ambapo watamchagua kiongozi mara moja katika kipindi cha miaka kumi
Pia ametoa onyo kali kwa wafisadi akisema kuwa ufisadi bado unaendelea kuwa tatizo kubwa nchini humo
Akihutubia zaidi ya wajumbe 2,000 mjini Beijing, bwana Hu alisema kuwa kukosa kushughulikia tatizo hilo, huenda kukasababisha pigo kubwa kwa chama.
Aidha Rais Hu anatazamiwa kujiuzulu kutoka wadhfa wake wa kiongozi wa chama na kumkabidhi Xi Ping anayeonekana kuwa kiongozi wa siku za usoni wa Uchina.
China ilipata mafanikio makubwa katika kipindi kilichopita ingawa changamaoto nazo zilikuwa nyingi.

Alitoa wito wa kuwepo malengo makubwa pamoja na kuhimiza bidii.
Hotuba yake ilifungua rasmi mkutano wa wiki moja utakaoshuhudia kuteuliwa kwa viongozi wapya wa chama.
Hali ya usalama imedhibitiwa mjini Beijing, huku wanaharakati wakiwa wamezuiliwa au kupewa kifungo cha nyumbani, kulingana na mashirika ya kibinadamu.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment