MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

THEO WALCOTT ASIFIWA NA WENGER



Meneja wa klabu ya soka ya Arsenal ya Uingereza, Arsene Wenger, amemsifu sana Theo Walcott, kwa kuichezea vizuri sana timu hiyo usiku wa Jumanne, katika mechi ambayo timu hiyo ilitoka sare ya 2-2 katika mechi ya ugenini dhidi ya Schalke ya Ujerumani. 

Walcott, ambaye mashauri ya kuongezewa mkataba yalivunjika mwezi Agosti, alianza vyema katika mechi hiyo, kwa kuifungia Arsenal bao la kwanza, na ikiwa ni mara ya nne msimu huu anapoingia katika mechi tangu mwanzo.

Lakini ilikuwa ni mara ya kwanza kucheza tangu mwanzo katika mechi ya Ulaya tangu mwezi Machi.

"Alicheza vizuri sana," alisema Wenger. "Alikuwa ni kati ya wachezaji wetu waliocheza vizuri sana."

Kulikuwa na wasiwasi kama Walcott angelicheza katika mechi ya jana, baada ya kuugua kwa muda, lakini kwa kutokuwepo Aaron Ramsey, ilibidia aingie uwanjani.


Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment