Kocha wa Arsenal Arsene Wenger , amekariri kuwa klabu hiyo haina nia yoyote ya kumuuza mchezaji wake Theo Walcott, msimu wa usajili Januari mwakani.
Kufuatia uamuzi huo, Arsenal, sasa huenda ikampoteza Walcott, mwenye umri wa miaka 23, ila kupokea chochote, kwa kuwa kandarasi ya mchezaji huyo inakamilika mwisho wa msimu huu.
Ikiwa Walcott na wasimamizi wa klabu hiyo hawataafikiana lolote, kabla ya wakati huo, Walcott atakuwa huru kuanzisha mazungumzo na klabu yoyote.

0 maoni:
Post a Comment