MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

BIA ya Safari Lager inayotengenezwa na kampuni ya bia ya Tanzania (TBL) imenyakua tuzo ya ubingwa wa jumla katika mashindano ya kwanza ya ubora wa bia yaliyoandaliwa na taasisi ya The Institute of Brewing and Distilling (IBD).
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam jana Meneja wa bia hiyo Oscar Shelukindo, alisema mashindano hayo yalifanyika kuanzia Machi tatu had inane mwaka huu katika jiji la Accra Ghana.
Alisema katika mashindano hayo yalishuhudia kampuni ya kutengeneza bia ya SABMiller Afrika ikipokea tuzo 10 kati ya 13 zilizotolewa ikiwamo tuzo hiyo ya ubingwa wa jumla.
“Bia ya Safari Lager inafahamika vizuri kwa ladha yake yenye ubora wa hali ya juu usiobadilika hili si jambo geni miongoni mwa Watanzania, lakini kutunikiwa tuzo ya ubingwa wa jumla katika mashindano yanayoshirikisha bia nyingi za bara la Afrika ni jambo la kutia for asana.
“Pamoja na hilo bia ya Safari Lager pia imenyakua tuzo ya ubora wa bia za Afrika zenye kiwango cha kilevi cha zaidi ya asilimia tano, hii inadhihirisha kwamba tumejizatiti katika umakini wa utengenezaji wa bia hii.
“Tuzo hii ya ubingwa wa jumla inawapa wateja wetu uhakika kwamba kweli wanakunywa bia bingwa,” alisema.
Alisema katika mashindano hayo zaidi ya bia 50 kutoka katika makampuni maarufu yanayotengeneza bia Afrika yalishiriki mashindano hayo yakiwamo makampuni kama SABMiller Afrika na SAB Ltd.
Aidha alisema katika mashindano hayo taasisi hiyo ya IB ilikusanya watalaam huru kutoka katika mabara matatu tofauti ili kuonja bia na kuto maamuzi yasiyo na upendelea wowote.
“Katika mashindano haya bia hizi zilipimwa katika makundi tofauti kama vile bia zinazotengenzwa kwa kutumia malighafi zinazopatikana sehemu inapotengenezwa bia yenyewe, bia zeny kiwango cha kilevi chini ya asilimia tano, na pia kundi la bia zenye kiwango cha kilevi cha zaidi ya asilimi tani,” Alisema.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment