MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG
                                            12,000 WAFUKUZWA KAZI.

Kampuni kubwa zaidi duniani ya madini ya Platinum, Anglo American Platinum, imewaachisha kazi wachimba migodi 12,000 waliokuwa wanagoma kudai nyongeza ya mishahara.

Kampuni hiyo, Amplats, ilisema kuwa mgomo haramu wa wiki tatu uliofanywa na takriban wachimba migodi 28,000 mjini Rustenburg, uliiletea hasara ya dola milioni 82.3.
Sekta ya madini nchini Afrika Kusini, imekumbwa na migomo ya wachimba migodi na hata kukatokea maafa baada ya polisi kuwapiga risasi zaidi ya wachimba migodi 30, waliokuwa wanagoma kutaka waongezwe mishahara.

Ikieleza sababu ya kuchukua hatua hiyo, Amplats, ilidokeza kuwa, wachimba migodi walikosa kuhudhuria vikao vya kinidhamu na ndiyo maana wakaachishwa kazi.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment