Waziri wa Mashauri ya nchi za Nje wa Marekani, John Kerry, amesema kuwa
mashambulio yaliyofanywa na wanajeshi wa kikosi maalumu cha Marekani nchini
Libya na Somalia yanaonesha dhamira ya serikali ya Marekani kuwasaka wale
wanaohusika na ugaidi.
Akizungumza nchini Indonesia, Bwana Kerry alisema Marekani
haitasita katika vita vyake dhidi ya ugaidi.
Jumamosi makamando wa Marekani walishambulia nyumba mjini
Barawe, Somalia, ambayo inadaiwa kutumiwa na kiongozi mmoja wa kundi la
al-Shabaab aliyehusika na shambulio la kigaidi katika jumba la maduka la
Westgate mjini Nairobi.
Baada ya mapambano makali ya risasi kikosi hicho cha Marekani
kiliondoka.
Haikuelezwa iwapo kiongozi huyo wa al-Shabaab aliuwawa au
kutekwa mjini Barawe.
Masaa machache baadae makamando wa Marekani walimkamata kiongozi
wa al-Qaeda katika mji mkuu wa Libya, Tripoli.
Anas al Libi alikuwa anasakwa kwa kuhusika na mashambulio dhidi
ya balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania miaka 15 iliyopita.
Inaarifiwa kuwa Anas al Libi sasa anazuwiliwa nje ya Libya.
Kutoka BBC
0 maoni:
Post a Comment