MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

MAREKANI YAINGIA BARAWE NA TRIPOLI

Anas al Libi
Waziri wa Mashauri ya nchi za Nje wa Marekani, John Kerry, amesema kuwa mashambulio yaliyofanywa na wanajeshi wa kikosi maalumu cha Marekani nchini Libya na Somalia yanaonesha dhamira ya serikali ya Marekani kuwasaka wale wanaohusika na ugaidi.

Akizungumza nchini Indonesia, Bwana Kerry alisema Marekani haitasita katika vita vyake dhidi ya ugaidi.
Jumamosi makamando wa Marekani walishambulia nyumba mjini Barawe, Somalia, ambayo inadaiwa kutumiwa na kiongozi mmoja wa kundi la al-Shabaab aliyehusika na shambulio la kigaidi katika jumba la maduka la Westgate mjini Nairobi.

Baada ya mapambano makali ya risasi kikosi hicho cha Marekani kiliondoka.
Haikuelezwa iwapo kiongozi huyo wa al-Shabaab aliuwawa au kutekwa mjini Barawe.

Masaa machache baadae makamando wa Marekani walimkamata kiongozi wa al-Qaeda katika mji mkuu wa Libya, Tripoli.

Anas al Libi alikuwa anasakwa kwa kuhusika na mashambulio dhidi ya balozi za Marekani nchini Kenya na Tanzania miaka 15 iliyopita.

Inaarifiwa kuwa Anas al Libi sasa anazuwiliwa nje ya Libya.
                                                               Kutoka BBC
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment