MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

YANGA KUFANYA MAANDAMANO SIKU YA JUMATATU



 Yanga kuandama jumatatu kudai kuongezewa eneo la kujenga uwanja
Baraza la Wazee wa Klabu ya Yanga, limetangaza kufanya maandamano makubwa siku ya Jumatatu ya Machi 17, endapo Manispaa ya Ilala itashindwa kuwajibu ombi lao la kuongezewa heka 11 katika eneo la Jangwani ili wajenge Uwanja wa kisasa wa michezo..............


Maandamano hayo yatashirikisha wanachama na wapenzi wa Yanga, kwa madai kuwa serikali imeshindwa kuwathamini na kutotambua mchango wao, licha ya klabu hiyo kujihusisha na mambo mengi ya kimaendeleo.

Katibu wa Baraza la wazee wa Yanga, Ibrahim Akilimali alifunguka na kusema kuwa “Yanga ni timu kubwa yenye historia nzuri na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivyo inashangaza kama leo kuna watu wanashindwa kutambua mchango wake na kuanza kutusumbua kwa mwaka mzima sasa.
 

“Tunatoa siku tano tano za serikali kwa kupitia Manispaa ya Ilala, chini ya Meya wake Jerry Silaa kujibu maombi
Uongozi wa Yanga kupitia Katibu mkuu wake Bw-Benny Njovu, umeitisha maandamano mach 17, mwaka huu siku a Jumatatu, na kumtaka  kamanda wa Polisi kanda maalum ya DSM,  Seleman Kova, kutoa Kibali cha maandamano hayo.

 Barua hiyo ilisema kuwa uamuzi wa kuitisha maandamano hayo umetokana na Manispaa ya Ilala kuchelewesha maombi yao ya kuongezewa eneo la ujenzi wa Uwanja, hivyo wao wameamua kuandamana kisheria.

Lakini alipotafutwa Kova, kuzungumzia swala hilo alisema kuwa yeye hakuwepo ofisini, hivyo hana jibu lolote juu ya maandamano hayo.

“Nipo nje ya Ofisi kwa siku nzima ya leo (jana), hivyo sijui lolote juu ya madai hayo,” alisema Kova.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment