Shirika la ndege la Kenya limetangaza kuwa litasimamisha
safari za ndege za kwenda Sierra Leone na Liberia kwa sababu ya ugonjwa wa
ebola ulioko Afrika Magharibi................
Imesema hatua hiyo itaanza kutekelezwa kutoka usiku wa
Jumaane.
Akizungumza kwenye mkutano huohuo wa waandishi wa habari
mjini Nairobi, mkurugenzi wa afya ya jamii, Nicholas Muraguri, alisema hakuna
raia kutoka nchi zenye ebola atayeruhusiwa kuingia Kenya.
Shirika la afya duniani, WHO, limesema Kenya iko katika
hatari ya ugonjwa wa ebola kuingia nchini humo, kwa sababu ni nchi ambapo
safari nyingi za ndege kutoka Afrika Magharibi zinatua.
WHO piya ilisema makisio ya ugonjwa huo ulivotapakaa siyo
kadiri ya hali halisi.
0 maoni:
Post a Comment