Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameapa kwamba
atawakabili vikali magaidi baada ya shambulio la kigaidi kuua watu zaidi ya 36
mjini Ankara.
Bw Erdogan amesema shambulio hilo lililotekelezwa
kupitia gari lililotegwa mabomu litazidisha kujitolea kwa maafisa wa usalama wa
Uturuki.
Mlipuko huo ulitokea katika kituo muhimu cha
uchukuzi cha Guven Park na kujeruhi zaidi ya watu 100. Mshambuliaji mmoja
anadaiwa kuuawa.
Waziri wa mambo ya ndani Efkan Ala alisema uchunguzi
utakamilishwa Jumatatu na kwamba wote waliohusika watatajwa.
Hakuna kundi lililokiri kuhusika lakini duru za
serikali zinashuku chama kilichopigwa marufuku cha Kurdistan Workers Party
(PKK).
kutoka BBC Swahili.
0 maoni:
Post a Comment