MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

ERDOGAN AAPA KUKABILI VIKALI MAGAIDI

Erdogan
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan ameapa kwamba atawakabili vikali magaidi baada ya shambulio la kigaidi kuua watu zaidi ya 36 mjini Ankara.

Bw Erdogan amesema shambulio hilo lililotekelezwa kupitia gari lililotegwa mabomu litazidisha kujitolea kwa maafisa wa usalama wa Uturuki.

Mlipuko huo ulitokea katika kituo muhimu cha uchukuzi cha Guven Park na kujeruhi zaidi ya watu 100. Mshambuliaji mmoja anadaiwa kuuawa.

Waziri wa mambo ya ndani Efkan Ala alisema uchunguzi utakamilishwa Jumatatu na kwamba wote waliohusika watatajwa.


Hakuna kundi lililokiri kuhusika lakini duru za serikali zinashuku chama kilichopigwa marufuku cha Kurdistan Workers Party (PKK).

kutoka BBC Swahili.
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment