Rais wa Rwanda Paul
Kagame amelaumu Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kutumia pesa ‘kiholela’
kutokana na mawaziri kufanya ziara za mara kwa mara kuhudhuria mikutano.
Amesema mawaziri wa
nchi yake wanatumia chombo hicho kama njia ya kujinufaisha kwa kufanya ziara na
kuhudhuria mikutano ya jumuiya hiyo isiyo muhimu.
Ameahidi kuiga mfano wa
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli kutokomeza ufisadi huo wa kusitisha ziara
za mawaziri alizotaja kuwa za kufuja mali ya taifa.
Akiongea katika mkutano
wa faragha wa viongozi wa taasisi zote za serikali nchini Rwanda, Rais Kagame
amesema suala la ufisadi nchini humo linachukua mwelekeo mpya na kasi ya ajabu
na kwamba hawezi kuendelea kuvumilia.
Rais Kagame aidha
amesema Jumuiya ya Afrika Mashariki imeanza kuwa ghali na mzigo kwa taifa lake
akisema mawaziri katika mataifa wanachama wanatumia jumuiya hiyo kama chombo
cha kuchota pesa kwa kubuni mikutano ya kila siku baadhi akiitaja kuwa haina
umuhimu wowote.
0 maoni:
Post a Comment