MWERA AMAZING BLOG

MWERA AMAZING BLOG

Kiongozi wa Mila: Kupatwa kwa jua ni ishara ya Mungu kumkubali Rais Magufuli

Katibu wa Mila wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya, Mwanasimtwa Mwagongo, amesema tukio la kupatwa kwa jua linalotarajiwa kutokea Alhamisi hii katika Kijiji cha Rujewa wilaya ya Mbarali, ni ishara ya Mwenyezi Mungu kuukubali uongozi wa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Magufuli.
553252_833275840056825_315738904966970792_n
Akizungumza jana na waandishi wa habari, habari za Utalii na Uwekezaji Tanzania (TAJATI) nyumbani kwake katika Kata ya Isisi, Mwagongo alisema tukio hilo la kupatwa kwa jua nchini si mkosi, bali ni sawa na taa iliyokuwa imezimika na sasa imewashwa na kuongeza, hii ishara kuwa Mungu ameukubali utawala uliopo madarakani na ndiyo sababu ametoa giza na kuleta nuru.
slide_4420_61964_large
“Hapo zamani watoto walikuwa hawaruhusiwi kutoka nje siku ya tukio hili, Wazee waliamini ni ajali ya kugongana jua na mwezi na wanaoumia ni wanadamu hasa watoto kwa kusababishiwa milipuko ya magonjwa mbalimbali,” alisema.

“Lakini kwa sasa tunatambua kuwa ni tukio la kisayansi na kutokea kwenye eneo letu ni neema kutoka kwa Mungu. Kupitia tukio hili dunia itaijua Tanzania, itaijua Mbarali na itaijua Rujewa. Ni tukio ambalo limetutangaza”.

Aidha Mwagogo alisema baada ya tukio hilo, wazee wa kimila watachinja ng’ombe kwa ajili ya kumshukuru Mungu kwa neema ya tukio hilo na pia kumwomba aiepushe jamii na madhara yoyote yanayoweza kujitokeza.

Aliwaasa viongozi wa dini zote kote nchini kuliombea tukio hilo ili lifanyike na kupita kwa amani na pasiwepo na uvunjifu wa amani utakaosababisha jamii kutoa tafsiri ya tofauti baada ya tukio hili la kihistoria ambalo litafanyika kati ya saa 4.15 asubuhi hadi saa 8.00 mchana.
CHANZO: HABARI LEO
Share on Google Plus

About MWERA AMAZING

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 maoni:

Post a Comment